the rising star
Monday, March 18, 2013
Ni Ambassadors Christ kwenye Tamasha la Pasaka,utakuwa wapi?
KUNDI la muziki wa kiroho la Ambassadors of Christ ‘Kwetu Pazuri’ la Kigali, Rwanda linatarajia kuzindua albamu mpya iitwayo Kaeni Macho, Machi 31, mwaka kwenye Tamasha la Pasaka.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema Dar es Salaam jana kuwa kundi hilo limemhakikishia kwamba albamu hiyo itakuwa moto wa kuotea mbali.
Alizitaja nyimbo zilizopo kuwa ni Kaeni Macho, Mungu Wangu, Tugireurukundo, Ewe Ndugu, Tuombeane, Umwamini Yesu, Msalaba, Twawona, Okuswala na Huruma.
“Kundi hilo maarufu kwa jina la Kwetu Pazuri, limefurahi sana kuja hapa Tanzania na wamenieleza albamu hiyo hawajawahi kuizindua hivyo ni baraka kubwa kwa Watanzania kupewa heshima hiyo,” alisema Msama na kuongeza kuwa kundi hilo pia litatumbuiza katika maonyesho mengine ya mikoani.
Kwa mujibu wa Msama hivi sasa kundi hilo linatamba na albamu ya Mtegemee Yesu na wamemhakikishia kuwa watang’arisha tamasha la mwaka huu na wamejipanga vya kutosha kuhakikisha mashabiki wanapata burudani ya nguvu.
Alisema albamu yao hiyo ina nyimbo nane ambazo ni JY’ Ushima Uwite, Mtegee Yesu, Ndifuza Kugerayo, Iyana Iby’ Isi, Yesu Niwe Mungeri, Parapanda, Abasaruzi na Nenda.
Licha ya kundi hilo, wasanii wengine wa nje ya Tanzania watakaotumbuiza tamasha hilo ni Sipho Makhabane wa Afrika Kusini, Ephraim Sekeleti wa Zambia na Solomon Mukubwa raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi Kenya.
Wasanii wa Tanzania waliothibitisha hadi sasa ni Rose Muhando, Upendo Nkone, John Lissu, Kwaya ya Kinondoni Revival na kundi la Glorious Celebration.
Tamasha la Pasaka litafanyika Dar es Salaam Machi 31, na litaendelea Aprili Mosi kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya, wakati Aprili 3 ni Uwanja wa Samora, Iringa, Aprili 6 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na siku inayofuata itakuwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Tuesday, November 20, 2012
HUKUMU YA FUNDIKIRA WATU WALIA NA KUZIMIA MAHAKANI.
Leo ilikuwa ndiyo siku ya hukumu dhidi ya watuhumiwa watatu wa mauaji ya marehemu Swetu Fundikira aliyeuawa kwa kupigwa miaka miwili iliyopita. Mara baada ya watuhumiwa hao kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa, ndugu na jamaa wa marehemu waliangua kilio na wengine hadi kuzimia kama walivyoshuhudiwa na paparazi wetu aliyeweka kambi mahakamani hapo. Kushoto ni dada wa marehemu Rehema Fundikira, Hadija Mdemu shemeji wa marehemu.
ndugu wakilia
Watuhumiwa wakiwa mahakamani kabla ya hukumu kusomwa. kutoka kulia ni Rhoda Robert, Ally Gube na Mohamed Ally.
Wednesday, November 7, 2012
KANGA NA MISEMO YAKE
KANGA NA MISEMO YAKE
USILAUMU SISIMIZI SAUKARI HAIMALIZI,
UTAUMIZA ROHO YAKO,
SIRI NI YA WAWILI
KANGA KAMA TUNAVYOJUA NI VAZI LA MWANAMKE WA KITANZANIA KAMA ILIVYOKITENGE, BATIKI,NA MAVAZI MBALIMBALI.
UZURI WA VAZI HILI LA KANGA HUONGEZWA NA MISEMO ILIYO IBEBA KWANI MISEMO
HII MBALI YA KUBURUDISHA PIA INAFUNDISHA KAMA IKITUMIWA VIZURI.
HIVYO WANAWAKE TULIENZI VAZI LETU HILI NA SI KULIDHARAU ,
MPENDA KWAO HUTUNZWA LOLEST,
OBAMA AWASHUKURU WAMAREKANI KWA KUMPA USHINDI
Akiwa na mkewe, Michelle, na binti zake Sasha (wa pili kulia) na Malia Obama wakisherehekea ushindi wake.
Romney akiwashukuru waliompigia kura.
ALIYEKUWA mgombea wa urais wa Marekani kupitia chama cha Democratic, Barack Obama, amemshinda mpinzani wake kutoka chama cha Republican, Mitt Romney, katika uchaguzi uliofanyika jana.
Obama ambaye alishinda urais wa nchi hiyo miaka minne iliyopita, amesema hivi sasa ana dhamira ya hali ya juu zaidi na nguvu zaidi za kufanya kazi zake. Aliyasema hayo huko Chicago wakati wa hotuba yake ya kupokea ushindi huo.
Hata hivyo, wagombea wote wawili wa kinyang’anyiro hicho walitoa wito wa umoja kwa watu wa nchi hiyo kwa ajili ya maendeleo.
Katika hotuba hiyo alimshukuru mkewe na mabinti zake , Sasha na Malia, ambao alisema ni “wasichana wawili jasiri kama mama yao.”
Katika uchaguzi huo Obama alipata kura nyingi hususani katika majimbo ya Ohio, Iowa, Wisconsin, Pennsylvania, New Hampshire na Virginia.
Kiongozi huyo alipongezwa haraka na viongozi wengine duniani wakiwemo David Cameron wa Uingereza na Benjamin Netanyahu.
Tuesday, October 9, 2012
hivi ni baadhi tu, ya yaliyojiri ndani ya fiesta 2012,
Diamond na vijana wake wakivua nguo jukwaani wakati wa shoo ya Fiesta 2012.
INAWEZEKANA kwamba Tamasha la Fiesta 2012, lilikumbwa na matukio mengi ya aibu lakini lile la mwanamuziki Nasibu Abdu Juma ‘Diamond’, kuvua nguo na kumwaga ‘lazi’ mbele ya maelfu ya Watanzania, likawa la funga kazi kuliko yote.
Diamond ambaye alishangiliwa vilivyo, wakati akitumbuiza na kudhihirisha kwamba yeye bado moto wa kuotea mbali anapokabidhiwa jukwaa, alipozidiwa na mzuka, alisaula suruali yake na kubakiwa na kivazi cha ndani ambacho wengi hukiita ‘boxer’ (chupi).
Mwanamuziki huyo, hakufanya hivyo peke yake, kwani aliposaula na wacheza shoo wake walimfanya vivyo hivyo, nao wakabakiwa na vi-boxer vyao.
Hawakuishia hapo, baada ya kuvua na kubaki hivyo, wakawapa migongo mashabiki na kuwachezea, hivyo kukamilisha zoezi la kumwaga ‘lazi’.
BABY MADAHA NAYE
Uchunguzi unaonesha kwamba mwanamuziki Baby Madaha alikuwa msanii aliyetumia muda mwingi kujiandaa na shoo ya Fiesta 2012. Hata hivyo, jukwaa lilimkataa kutokana na mpangilio wa ratiba, kwa hiyo akabaki amejikunyata ‘back-stage’ wakati wasanii wenzake wakipanda jukwaani na kufanya kazi zao.
Kwa upande mwingine, wasanii wa kiume walimuona kama ‘kiburudisho’ chao, kwani walipojisikia, walimvaa, wakamkumbatia na kumpiga mabusu.
Hili la kumkumbatia na kumpiga mabusu, lilichukuliwa kama ni la kumfariji lakini wengine hususan wanamuziki wa kiume, walisema wanaona burudani kumkumbatia na kumbusu.
KUNA WAREMBO WALITWANGANA
Gari aina ya Mercedes Benz, lililombeba mwanamuziki wa Kimarekani, Rick Ross, lilipoingia uwanjani, warembo wawili walijikuta wakiwashiana moto, kila mmoja akimsema mwenzake kuwa ana kiherehere.
Warembo hao, kila mmoja alikuwa anataka kulishika gari hilo kwa lengo la kumfikia Rick Ross ‘The Boss’ lakini katika kile ambacho wengi walikiona ni cha ghafla, wao kwa wao walishikana.
Hata hivyo, warembo hao waliamuliwa na kuondolewa uwanjani hapo, hivyo kuambulia sifuri, kwani siyo tu kwamba walishindwa kumfikia mwanamuziki huyo, bali pia hata shoo yake hawakuiona.
TATHMINI YA JUMLA
Fiesta 2012, limekuwa na mafanikio zaidi kutokana na kumshusha nchini msanii ambaye anakubalika zaidi ulimwenguni kwa kipindi hiki. Rick Ross, yupo kwenye orodha ya wanamuziki wa Hip Hop daraja la kwanza kwa sasa ndiyo maana ujio wake, umeweza kuongeza chachandu ya aina yake kwenye Fiesta. Lingine ni kwamba Diamond aliweza kuwavalisha nguo wanamuziki wake wa safu ya kuimba, kwani kabla hawajapanda, walionekana wakiwa hawana jipya.
Wanamuziki wa Hip Hop, waling’ara vizuri kwenye Fiesta ya mwaka huu.
INAWEZEKANA kwamba Tamasha la Fiesta 2012, lilikumbwa na matukio mengi ya aibu lakini lile la mwanamuziki Nasibu Abdu Juma ‘Diamond’, kuvua nguo na kumwaga ‘lazi’ mbele ya maelfu ya Watanzania, likawa la funga kazi kuliko yote.
Diamond ambaye alishangiliwa vilivyo, wakati akitumbuiza na kudhihirisha kwamba yeye bado moto wa kuotea mbali anapokabidhiwa jukwaa, alipozidiwa na mzuka, alisaula suruali yake na kubakiwa na kivazi cha ndani ambacho wengi hukiita ‘boxer’ (chupi).
Mwanamuziki huyo, hakufanya hivyo peke yake, kwani aliposaula na wacheza shoo wake walimfanya vivyo hivyo, nao wakabakiwa na vi-boxer vyao.
Hawakuishia hapo, baada ya kuvua na kubaki hivyo, wakawapa migongo mashabiki na kuwachezea, hivyo kukamilisha zoezi la kumwaga ‘lazi’.
BABY MADAHA NAYE
Uchunguzi unaonesha kwamba mwanamuziki Baby Madaha alikuwa msanii aliyetumia muda mwingi kujiandaa na shoo ya Fiesta 2012. Hata hivyo, jukwaa lilimkataa kutokana na mpangilio wa ratiba, kwa hiyo akabaki amejikunyata ‘back-stage’ wakati wasanii wenzake wakipanda jukwaani na kufanya kazi zao.
Kwa upande mwingine, wasanii wa kiume walimuona kama ‘kiburudisho’ chao, kwani walipojisikia, walimvaa, wakamkumbatia na kumpiga mabusu.
Hili la kumkumbatia na kumpiga mabusu, lilichukuliwa kama ni la kumfariji lakini wengine hususan wanamuziki wa kiume, walisema wanaona burudani kumkumbatia na kumbusu.
KUNA WAREMBO WALITWANGANA
Gari aina ya Mercedes Benz, lililombeba mwanamuziki wa Kimarekani, Rick Ross, lilipoingia uwanjani, warembo wawili walijikuta wakiwashiana moto, kila mmoja akimsema mwenzake kuwa ana kiherehere.
Warembo hao, kila mmoja alikuwa anataka kulishika gari hilo kwa lengo la kumfikia Rick Ross ‘The Boss’ lakini katika kile ambacho wengi walikiona ni cha ghafla, wao kwa wao walishikana.
Hata hivyo, warembo hao waliamuliwa na kuondolewa uwanjani hapo, hivyo kuambulia sifuri, kwani siyo tu kwamba walishindwa kumfikia mwanamuziki huyo, bali pia hata shoo yake hawakuiona.
TATHMINI YA JUMLA
Fiesta 2012, limekuwa na mafanikio zaidi kutokana na kumshusha nchini msanii ambaye anakubalika zaidi ulimwenguni kwa kipindi hiki. Rick Ross, yupo kwenye orodha ya wanamuziki wa Hip Hop daraja la kwanza kwa sasa ndiyo maana ujio wake, umeweza kuongeza chachandu ya aina yake kwenye Fiesta. Lingine ni kwamba Diamond aliweza kuwavalisha nguo wanamuziki wake wa safu ya kuimba, kwani kabla hawajapanda, walionekana wakiwa hawana jipya.
Wanamuziki wa Hip Hop, waling’ara vizuri kwenye Fiesta ya mwaka huu.
Wednesday, October 3, 2012
HIVI NDIVYO BIRTHDAY YA DIAMOND ILIVYOKUWA NDANI YA D'MAGE HOTEL USIKU WA JANA
DIAMOND NA WASAFI.......
mapenzi ni kikohazi kulicha huliwezi..........
HAPPY BIRTHDAY DIAMOND
Hii ni cake maalum ambayo aliletewa na Wema kama moja ya zawadi ya Birthday yake |
Hapa akiwa na Dada yake wa hiyari Halima kimwana |
Wema na dada yake Diamond Esma wakilishana Cake |
mapenzi ni kikohazi kulicha huliwezi..........
All de way from UK Naj pia alikuwepo |
Dimpoz kwa Poz, Mboni Masimba na Mecky |
Hapa tukiwa na Roho ya Wolper Legraa Dallas |
Bhaaaaaaasssssssss....! |
Joff mnyama pia ndani |
Hapa babtale na Naj wakiteta jambo |
Team sheta pia Ndani.... |
Weeeeeeeeeeeeee.........! |
Dallas tena...... |
gift from wema
Hapa wema na Mboni masimba |
Kama ulikua haujui hawa ndio vijana wanaoongoza kwa Kuvimba mjini........LOL! |
All de way from America Wasafi walikua ndani pia...... |
HAPPY BIRTHDAY DIAMOND
DOZEN & SHETTA |
Watoto wa ManzeseTIPTOP pia ndani |
Watuacheeeeee na Mama yangu mboni ali masimba....... |
Subscribe to:
Posts (Atom)